JUKWAA LA HABARI

Latest Post

Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH, Dokta Amos Nungu amesema taarifa ya utafiti huo haikuwafikia
Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania ( COSTECH) imesikitishwa na kuvuja mitandaoni kwa mawasiliano ya barua iliyoiandikia Taasisi ya utafiti isiyo ya Kiserikali ya TWAWEZA.
Barua hiyo kuhusu kulitaka Twaweza litoe maelezo ndani ya siku saba kuhusu utafiti ulioifanya wa Sauti za Wananchi bila ya kibali, ambao umeonesha pia kushuka kwa uungaji mkono wa wananchi kwa wawakilishi waliowachagua.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa tume hiyo Dokta Amos Nungu amesema wameshangazwa kuona mawasiliano halali ya kiofisi yamesambazwa mitandaoni hata kabla ya kupata majibu rasmi.
Matokeo hayo ya utafiti, ndiyo yaliyoifanya Tume ya Sayansi na Teknolojia, ambayo ndiyo yenye jukumu la kuratibu, kufanya tathmini na ufuatiliaji wa tafiti, kuiandikia barua taasisi hiyo ya TWAWEZA, inayoonesha pia kwamba taasisi hiyo awali iliwasilisha maombi ya vibali vya kufanya utafiti nchini, lakini utafiti huo wa Sauti ya Wananchi haukujumuishwa.
Maelezo ndani ya barua hiyo imeitaka taasisi hiyo pia kutoa maelezo ndani ya ndani ya siku Saba.
'Mtafiti akija kutoa matokeo ya utafiti kwenye vyombo vya habari pia tunaona kuwa utafiti ulifanyika, huu utafiti tunakiri kuwa hatuna taarifa yake sababu mtafiti anaposajiliwa mwishoni anapoondoka na taarifa zake lazima ripoti ibaki COSTECH.Tumewaomba wiki moja watupe maelezo'' Dokta Amos Nungu, Kaimu Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia.
Na kuhusiana na hatua gani watakazochukua juu ya mawasiliano hayo ya ndani kusambaa mitandaoni, amesema hilo ni jukumu la Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.
''tume inasikitika kuwa mawasiliano halali ya kiofisi yanapelekwa mitandaoni tumeziachia mamlaka kufanya kazi yake''.Alieleza Dokta Nungu
TWAWEZA imekiri kupokea barua kutoka COSTECH ''tumeipokea na tunaifanyia kazi. Twaweza haijasambaza, na haihusiki na usambazaji wa barua hiyo kwenye mitandao ya kijamii.
Barua yoyote inayofika Twaweza inagongwa muhuri wa kupokelewa mbele ya mjumbe aliyeleta barua hiyo. Barua inayosambaa mtandaoni hatuitambui kwa sababu haina muhuri wetu wa kuipokea Twaweza. Tunaheshimu na kuthamini sana mawasiliano yetu na wadau wetu''Alieleza Aida Eyakuze Mkurugenzi mtendaji wa TWAWEZA
source: https://www.bbc.com/swahili


http://www.cefc.com.hk/wp-content/uploads/2015/01/communication_sin300_37118315.jpg

Rais wa China Xi Jinping ametaka kuwepo uvumilivu kutoka pande zote wakati wa mawasiliano ya simu na rais wa Marekani Donald Trump siku moja baada ya Korea kusema kuwa ilikuwa tayari kuzamisha meli ya kubeba ndege za vita ya Marekani.
Mawasiliano hayo ya simu ndiyo ya pili kati ya viongozi hao wawili tangu wakutane huko Florida mapema mwezi huu.
Ni ishara ya hofu ya China kuwa msukosuko kati ya Marekani na Korea Kaskazini utasababisha mzozo.
Siku ya Jumapili vyombo vya habari nchini Korea Kaskazini vilisema kuwa jeshi la Korea Kaskazini lilikuwa tayari kuzamisha meli ya Marekani ya USS Carl Vinson, ambayo Marekani inasema itawasili katika rasi ya Korea siku chache zinazokuja.
Meli hiyo ilitumwa na Rais Trump huku onyo ikitolewa kuwa Marekani imepotza uvumilivu kwa mipango ya nuklia ya Korea Kaskazini.
Wakati wa mazungumzo hayo ya simu Bwana Xi alitaka pande zote kuwa wavumulivu na kuzuia vitendo ambavyo vimaweza kuzua mzozo.
Ikulu ya White House inasema kuwa bwana Trump amesisitiza kuwa vitendo vya Korea Kaskazini vinavuruga rasi wa Korea.
 Viongozi hao walikutana kati ya tarehe 7 na 8 huko Florida na baada kuzungumza kwa njia ya simu kuhusu Korea Kaskazni tarehe 12 mwezi Aprili.
source; bbc/swahili

Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Thomas Emmanuel Ulimwengu anatarajiwa kuwa nje kwa miezi mitatu kutokana na maumivu ya goti la mguu wake kushoto. Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Eskilstuna nchini Sweden, Ulimwengu amesema kwamba amepokea taarifa za kusikitisha kutoka kwa Daktari wa timu yao.
"Juzi nilikwenda kupimwa na jana nikakutana na Daktari, maana nilivyoshitua goti kwenye mechi ya kirafiki nilianza maozezi ila bado ukawa unaendelea kuuma, hivyo jana ndiyo nimepewa hizi taarifa,"amesema Ulimwengu.Thomas Ulimwengu atakuwa nje kwa miezi mitatu kutokana na maumivu ya goti la mguu wake kushoto
Amesema ameambiwa anatakiwa kuwa nje kwa miezi mitatu kutokana na maumivu ya goti, baada ya vipimo alivyofanyiwa juzi nchini humo kufuatia kuumia Machi 23, akicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Malmo FF.Hakika huu ni mwanzo mbaya kwa Ulimwengu aliyejiunga na Eskilstuna Januari mwaka huu kutoka TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Ulimwengu aliyezaliwa Juni 14, mwaka 1993 aliibukia katika taasisi ya soka Tanzania (TSA) mwaka 2008, kabla ya mwaka 2009 kwenda kuanza kukomazwa Ligi Kuu katika klabu ya Moro United alikokuwa akicheza kwa mkopo hadi mwaka 2010 alipokwenda akademi ya AFC Eskilstuna ya Sweden, alikocheza hadi mwaka 2011 alipochukuliwa na timu ya vijana ya Mazembe.
Alicheza U-20 ya Mazembe kwa msimu moja kabla ya kupandishwa rasmi timu ya wakubwa mwaka 2012 na moja kwa moja kuwa mchezaji wa kikosi cha kwanza hadi anamaliza Mkataba wake Oktoba mwaka jana.Ulimwengu amehamia Ulaya baada ya kushinda mataji makubwa akiwa na Mazembe kama Ligi ya Mabingwa Afrika, Super Cup ya Afrika na pamoja na kucheza Klabu Bingwa ya Dunia.

Bingwa wa kutoa motisha afariki Afrika Kusini

Afrika Kusini inaomboleza kifo cha Ontlametse Phalatse, msichana wa umri wa miaka 18 ambaye alikuwa anaishi na ugojwa unaojulikana kama Progeria, ambayo ni hali ya kimaumbile isiyo ya kawaida ambayo husababisha mtu kuzeeka kwa haraka.
Mwezi uliopita Ontlametse alisherehekea siku ya kuzaliwa na rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma.
Seriklia ya Afrika kuisni imeongoza taifa kutuma rambi rambi kufuatia kifo hicho.
Alifariki hiyo jana katika hospitali ya Dr George Mukhari Academic iliyo nje ya mji wa Pretora.
Phalatse alikuwa mmoja wa wasichana wawili waliokuwa na hali hiyo nchini Afrika Kusini.
Alijiita "mama wa kwanza" , baada ya kuwa mtoto wa kwanza mweusi nchini Afrika Kusini, kupatikana akiwa na ugonjwa wa Progeria.
Alitajwa kuwa mtoto wa kuwapa watu motisha na mtot wa miujiza baada ya kuishi kuliko matarajio walioyokuwa nayo madaktari waliosema kuwa angefariki miaka minne iliyopita.
Rais Zuma ametuma rambi rambi zake kwa familia ya msichana huyo.
Bingwa wa kutoa motisha afariki Afrika Kusini
source:www.bbc.com/swahil

Rais wa Tanzania John Magufuli leo hii ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa awamu ya kwanza ya mradi mkubwa wa reli ya kisasa ya Standard Gauge ambayo hapo baadae itaunganisha nchi za Rwanda na Burundi pia.
Lakini katika awamu hii ya kwanza, ujenzi utakuwa wa reli yenye urefu wa kilomita takribani 300, ambayo itatoka jijini Dar es Salaam na kuishia mkoa wa jirani wa Morogoro.
Ni reli ya kisasa, na ya kwanza Afrika Mashariki na kati itakayokuwa na uwezo wa kupitisha treni zitakazoendeshwa kwa nguvu ya umeme.
Reli hiyo itajengwa kwa awamu ya kwanza na kampuni kutoka nchi mbili, uturuki na Ureno kwa gharama ya takriban dola bilioni 1.2 za Kimarekani.
Reli hiyo itakuwa na uwezo wa kubeba treni yenye kuvuta mabehewa 100 na kubeba mzigo wa mpaka tani 10000 kwa mkupuo sawa na uwezo wa Malori 500 ya mizigo.
Mradi huu utaleta ahueni kwa wasafiri wa Dar es Salaam mpaka Morogoro ambpo wataweza kusafiri kwa mwendo kasi kwa saa 2 na dakika 50 pekee
Rais wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli katika sherehe hizo amesema kuwa Tanzania itanufaika kutokana na Mradi huu kwa maendeleo ya uchumi,
Hivi sasa Serikali ya Tanzania inaelekeza jitihada zake za ujenzi wa reli wa awamu ya pili yenye urefu wa kilometa 336 kutoka Morogoro mpaka Dodoma yalipo makao makuu ya nchi na tayari serikali ya Uturuki imeonyesha nia ya kushirikiana na Tanzania kujenga sehemu hiyo.

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget