Articles by "Teknologia"



Image result for hacking

Polisi nchini Uhispania wamemtia mbaroni mtaalam wa kompyuta kutoka Urusi kwa madai ya kudukua mitandao wakati wa uchaguzi marekani, habari kutoka vyombo vya habari vya Uhispania vimesema. Pyotr Levashov, ambaye alishikwa tarehe 7 Aprili, kwa sasa amewekwa rumande. Shirika la habari la AFP pia ilijulishwa kwamba Marekani ilikuwa imetoa ombi la Levashov kurudishwa nchini humo. Ombi hilo litapelelezwa na mahakama ya jinai ya Uhispania, AFP iliongezea. El Confidencial, tovuti ya habari Uhispania ilisema kuwa hati ya kukamatwa kwa Levashov ilitolewa na Marekani kwa kile kilichokisiwa kuwa kudukua mitandao hatua iliodaiwa kusaidia kampeni ya Trump.
source: http://www.bbc.com/swahili/habari-39558269

Image result for Nokia 3310

Kuna taarifa kwamba huenda simu muundo wa Nokia 3310 zikazinduliwa upya na kuanza kuuzwa tena .
Kampuni ya HMD Global Oy ya Finland, ambayo ina haki za kuunda bidhaa za nembo ya Nokia ndiyo inayodaiwa kuwa na mipango hiyo.Simu hizo inaarifiwa zitazinduliwa wakati wa Kongamano la Simu za Rununu Duniani baadaye mwezi huu.Kampuni ya Nokia ilinunuliwa na Microsoft mwaka 2013.Simu asilia za Nokia 3310 zilipata umaarufu kutokana na uthabiti wake.Nokia 3310/3330, zilizinduliwa 2000, na ni miongoni mwa simu zilizouzwa sana duniani. Jumla ya simu 126 milioni za aina hiyo zilitengenezwa na Nokia.
Kilicho ongezeka kwenye simu mpya za Nokia 3310.


sorce:bbc/swahili

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget